WHATSAPP KUTUMIWA BURE >>>> SOMA ZAIDI HAPA>>>
Wamiliki wa app ya mawasiliano ya
WhatsApp wamefuta ada ambayo watumizi wake wamekuwa wakitakiwa kulipa
kila baada ya mwaka mmoja.
Ada hiyo ilianza kutozwa miaka michache iliyopita lakini kampuni hiyo inasema haijakuwa na manufaa sana.
Taarifa kutoka kwa wamiliki wa WhatsApp inasema: “Watu wengi wanaotumia WhatsApp hawana kadi za benki na wengine huwa na wasiwasi kwamba baada ya mwaka mmoja watazuiwa kuungana tena na marafiki na jamaa.”
“Kwa hivyo, wiki chache zijazo, tutaondoa ada zote tunazotoza wa wanaotumia aina mbalimbali za app yetu na hutatozwa tena pesa ili kutumia WhatsApp.”
Kwa sasa, WhatsApp, ambayo humilikiwa na Facebook, hutumiwa na watu bilioni moja na kampuni hiyo inatumai kuondolewa kwa ada kutavutia watu wengi zaidi.
Kwa sasa WhatsApp hutumiwa na watu zaidi ya bilioni moja Lakini bado wamesisitiza kwamba hawatakuwa wakiweka matangazo na badala yake watatafuta njia nyingine za kujipatia mapato.
KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPO CHINI
Comments
Post a Comment