Posts

Showing posts with the label AFYA

Jinsi Vyakula Vinavyosababisha Magonjwa

Image
Jinsi Vyakula Vinavyosababisha Magonjwa Jarida la Emerging Infectious Diseases linasema kwamba zaidi ya magonjwa 200 yanaweza kusababishwa na chakula. Hata hivyo, vijidudu vinavyosababisha magonjwa hayo yote si vingi sana. Huenda takwimu zifuatazo zinaweza kufanya mtu afikiri hivyo. Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), kila mwaka watu milioni 130 hivi katika Eneo la WHO huko Ulaya wanaambukizwa magonjwa yanayosababishwa na chakula. Katika mwaka wa 1998, zaidi ya watu 100,000 nchini Uingereza walikuwa wagonjwa kwa sababu ya kula chakula kibaya, na 200 kati yao walikufa. Inakadiriwa kwamba kila mwaka watu milioni 76 hivi wanapata magonjwa yanayosababishwa na chakula huko Marekani, na 325,000 kati yao hulazwa hospitalini, na 5,000 hufa. Si rahisi kujua hesabu kamili ya ulimwenguni pote. Hata hivyo, shirika la WHO linaripoti kwamba watu milioni 2.2 hivi walikufa kutokana na magonjwa ya kuharisha katika mwaka wa 1998, na milioni 1.8 kati yao walikuwa wat...

Faida za Kiafya za Kunywa Maji ya Moto

Image
                         Faida za Kiafya za Kunywa Maji ya Moto   NJIA SITA ZA KUNYWA MAJI YA MOTO ZINAZOTIBU MWILI WAKO. Kunywa kikombe kimoja cha maji ya moto kila asubuhi inaweza kukutibu mwili wako kwa kusaidia umeng’enywaji wa chakula na kuzuia kuzeeka mapema kabla ya wakati. Wengi wetu huianza asubuhi vyema kwa kikombe safi cha kawaha ya moto au chai ya moto kwa lengo la kuuchangamsha miili yetu baada ya kutoka kitandani. Pale tunakunywa maji, basi wengi wetu hupendelea kunywa ya baridi, lakini kutokana na watalaam wa afya wanavyosema,  tunafanya makosa kufanya hivyo. Mara nyingi unywaji wa maji moto au uvuguvugu, hususani majira ya asubuhi, inasaidia kuiponya miili yetu na kuitibu,  kwa kusaidia kuongeza nguvu katika mmeng’enyo wa chakula ma kupunguza taka mwili ambazo zinaweza kuzuia kinga zetu kuwa katika hali yake nzuri ...

WALAJI WA NYAMA YA NGURUWE HATARINI KUUGUA KIFAFA

Image
WALAJI WA NYAMA YA NGURUWE HATARINI KUUGUA KIFAFA Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Kimehadhalisha walaji wa nyama ya Nguruwe nchini kuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata kifafa. Utafiti wa kisayansi uliofanywa na SUA umebaini kuwa baadhi ya Nguruwe wana minyoo aina ya Tegu ambao nyama yao ikiliwa bila kuiva vizuri, mlaji atapata minyoo hiyo ambayo huingia kichwani na kusababisha kifafa. Mhadhiri na Mtafiti Idara ya sayansi ya Wanyama na Uzalisha ya SUA, Profesa Faustine Lekule, alisema sampuli za utafiti huo kutoka Mbeya zimebaini Nguruwe wakiwamo wanaosafirishwa katika miji mikubwa wameathirika na minyoo hiyo. Kwa mujibu wa Prof. Lekule, wataalamu wa SUA wanaosimamia mradi wa utafiti wa kuboresha ufugaji wa Nguruwe kwa mkoa wa Mbeya ili kuinua pato la kaya, unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Denmark (DANIDA), walibaini hatari hiyo baada ya kuchukua sampuli ya nyama ya Nguruwe kwa ajili ya vipimo. "Majibu ya Sampuli ambazo wataala...
Image
UTAFITI: ULAJI WA MIRAA UNAPUNGUZA NGUVU ZA KIUME Ulaji wa Miraa unaathiri nguvu za kiume. Utafiti uliofanywa kwa niaba ya serikali ya Kenya na wahadhiri wa chuo kikuu cha Moi kilichoko katika Bonde la ufa umebaini kuwa Majani ya miraa inayofahamika pia kama 'Mairungi' unazuia ukuaji wa manii. Aidha ulaji wa kipindi kirefu wa miraa unafanya mbegu za kiume za wanaume kufa haraka pindi zinapowekwa kwenye uke. Mtafiti mkuu wa chuo kikuu cha Moi, Ochiba Lukanda, anasema kuwa utafiti sawa na huo uliofanywa huko ghuba ulibaini matokeo kama hayo. Lukanda anasema kuwa wanaume ambao wamekuwa wakila Miraa kwa kipindi kirefu na wakaacha huwa wanapata uwezo wao wa kutunga mimba. Ulaji wa Miraa pia huwa unasababisha mshtuko wa moyo. ''Mtu anapokula mmea huu baada ya muda damu yake huaanza kwenda kwa kasi, mbali na shinikizo la damu mumea huu hausababishi saratani kama inavyodaiwa '' Dakta Lukanda Hata hivyo utafiti katika maeneo yanayokuzwa mum...

Mapunye na athari kwa ngozi yako

Image
Ni matumaini yangu kuwa hamjambo wapenzi wasikilizaji na karibuni katika kipindi kingine cha Ijue Afya Yako. Katika kuhitimisha kujadili maradhi ya ngozi leo tunaangalia maradhi ya fangasi ya mapunye yanayoshambulia kichwa ambayo kitaalamu huitwa Tinea capitis. Aina hii ya maradhi ya fangasi hushambulia eneo la kichwa pekee ukiacha eneo la uso. Kwa maneno mengine, aina hii ya fangasi haishambulii uso bali eneo lililobaki la kichwa. Lakini je, mapunje huwashambulia kina nani zaidi? Ugonjwa huu hushambulia watu wote wa jinsia na umri wote, ingawa huonekana zaidi kwa watoto wadogo. Fangasi hawa hushambulia watoto wadogo ambao hawajafikia umri wa balehe na mara nyingi huacha kushambulia pale mtoto anapofikia umri huo wa balehe. Iwapo unataka kujua muonekano wa maradhi haya, unapaswa kujua kuwa, mapunye huweza kushambulia eneo zima la kichwa au sehemu tu ya kichwa. Eneo la ngozi ambalo lina mashambulizi ya mapunye huwa na umbo linalofanana na sarafu. Eneo hili la ngozi lil...

Tamko La Shirikisho La Vyama Vya Tiba Asili Tanzania (shivyatiata) Kuhusu Maelezo Ya Waziri Wa Afya Aliyoyatoa Tarehe 15/01/2016, Juu Ya Tiba Asili Natiba Mbadala.

Image
Ndugu waandishi wa Habari na ndugu wananchi, shirikisho la vyama vya Tiba Asili Tanzania (shivyatiata) ni chombo kinachosimamia vyama vyote vya Tiba Asili hapa Nchini pamoja na Waganga wote wa Tiba Asili na pia ndiyo msemaji wao kwa Serikali, Mashirika ya Kitaifa na Kimataifa na kuhakikisha chombo hiki kinasimamia na kulinda maslahi yote ya Waganga wa Tiba Asili hapa nchini Hivyo basi ,kutokana na maelezo yaliyotolewa na Waziri mwenye dhamana na mambo ya Afya mnamo hiyo tarehe 15/01/2016 shirikisho kwa kutambua dhamana tuliyonayo mbele ya Umma wa Waganga tunapenda kuwasilisha tamko letu kwenu nyinyi waandishi wa Habari na wanchi kwa ujumla ili muweze kuelewa yanayoendelea katika Tiba Asili hapa nchini. Ndugu waandishi wa Habari, kwanza mtakumbuka kuwa mnamo tarehe 14/12/2015 Naibu waziri wa Afya maendeleo ya Jamii, jinsia, wazee na watoto Mhe. Dkt HAMISI KIGWANGALA (MB) alifanya ziara katika kituo cha Tiba Mbadala cha Tabibu anayejulikana kwa jina la Dr MW...

MKURUGENZI MKUU WA TFDA,AWAHASA WATANZANIA KUHUSU MATUMIZI YA CHAKULA,SOMA HAPO KUJUA

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Hiiti Sillo akizungumza na waandishi wa habari juu ya uhamasishaji wa masuala ya Chakula Salama iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. WANANCHI wametakiwa kuangalia usalama wa chakula ili kuweza kuepuka vimelea vya viini vya magonjwa yanayotokana na kula chakula kisicho salama. Hayo ameyasema jana Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakulana Dawa (TFDA),Hiiti Sillo wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya uhamasishaji masuala ya usalama wa Chakula, amesema kula chakula chenye usalama inafanya kuwa taifa la maendeleo kiuchumi. Amesema kuwa chakula ni muhimu kwa maisha ya binadamu kwa kula chakula ambacho hakijachafuliwa na viini vya magonjwa kama, kuhara,kipindupindu. Sillo amesema watu milioni 91 duniani wanaugua magonjwa kutokana na kula chakula kilichochafuliwa na viini vya vimelea magonjwa. Amesema TFDA licha kuwa na changamoto lakini wameweza kuwa na mafanikio kwa kuweka watendaji mipakani pamoja...

HIV Status » Huddah Monroe » HUDDAH MONROE Finally Reveals Her HIV Status! You Will be Surprised

Image
HUDDAH MONROE Finally Reveals Her HIV Status! You Will be Surprised While marking World AIDs Day yesterday, Huddah Monroe decided to let Kenyans know her HIV status and let the world see as she takes her test and share her results. While many would expect her to be sick due to the high number of men she sleeps with, Huddah is HIV negative. Here is what she posted after taking the test; Hapy(sp) NEW month to all of you …. Plus ,It’s WORLDS AIDS DAY! As usual This is a day where by people world wide unite in the fight against HIV, show their support for people living with HIV and to commemorate people who have died…….Lots of people in the other hand dunno the facts about protecting themselves and others ,Stigma and discrimination still remains vital for some people living with the virus…. World AIDS Day is important because it reminds the public and Government that HIV has not gone away, there is still a vital need to raise money, increase awareness, fight prejudice and improve...