Misri yatofautiana na IS kuhusu shambulio
Rais Abdel Fattah al Sisi
Kundi la Islamic
State limekiri kutekeleza shambulio katika mji wa Cairo nchini Misri
ambalo liliwaua takriban watu tisa wengi wao wakiwa maafisa wa polisi.
Zaidi ya watu 13 walijeruhiwa akiwemo afisa mkuu wa polisi katika eneo la Giza,ambalo liko karibu na eneo maarufu lenye piramidi.
Serikali imeimarisha usalama huku taifa hilo likikaribia kuadhimisha miaka mitano ya mapinduzi yaliomuondoa rais wa muda mrefu wa taifa hilo Hosni Mubarak.
Vuguvugu la Muslim brotherhood,ambalo ndilo lililomuweka aliyekuwa rais Mohammed Morsi ambaye alichagliwa baada ya mapinduzi ilipigwa marufuku.
Comments
Post a Comment