Man Utd wakana kukutana na Guardiola

PepGuardiola ataondoka Bayern baada ya kumalizika kwa msimu huu                                                     

Manchester United wamekanusha habari kwamba walikutana na kuzungumza na meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola kuhusu uwezekano wake kuwa meneja wao.
Tovuti ya France Football ilikuwa imesema mkutano huo ulifanyika mjini Paris lakini United wamesema habari hizo si za kweli.
Meneja wa sasa wa United Louis van Gaal amekabiliwa na shinikizo baada ya klabu hiyo kutofanya vyema ligini Uingereza na Ulaya..
  • Guardiola asema atahamia Uingereza
Guardiola, 45, anataondoka Bayern Munich majira yajayo ya joto na amesema amepokea maombi kutoka kwa klabu kadha za Uingereza.
Manchester City wamo kwenye nafasi nzuri ya kumchukua, lakini Chelsea na United wamedaiwa kumtafuta pia.
Bayern Munich walikuwa kwenye kambi ya mazoezi Doha wakati wa mapumziko ya msimu wa baridi na watarejea kucheza Ijumaa dhidi ya Hamburg.

Comments

Popular posts from this blog

TAZAMA PICHA 30 ZA MREMBO AGNES MASOGANGE AKIJIACHIA KISTAA NJE YA NCHI

Gamboshi: Makao Makuu ya Uchawi na Wachawi yaliyopo Shinyanga, Tanzania

14 parties want Parliament to discuss Zanzibar impasse