Kimbunga kikali chawasili Marekani mashariki

Ajali zilizosababishwa na kimbunga hicho                                                                                           

Kimbunga kikali cha theluji kinachobashiriwa kuwa kikubwa zaidi kwa muda wa miaka mia moja kimewasili katika ufukwe wa Mashariki mwa Marekani.

Eneo linalotarajiwa kukabiliwa vikali ni mji mkuu wa Washington DC, ambako hali ya hatari tayari imetangazwa.

Afisi za wafanya kazi wa Serikali na shule zilifungwa mapema na huduma za usafirishaji pia kusitishwa.


Kimbunga nchini Marekani                                                                                                                   
 
Mwandishi wa BBC alisema kuwa mji huo ni kama uliohamwa kwa kuwa watu wote wamejifungia manyumbani hadi kimbunga hicho kitakapopita.

Mji wa New York pia umetangaza hali ya hatari ya hali ya hewa.

Kumekuwa na visa zaidi ya 1,000 vya magari kugongana katika Caroline Kaskazini pekee.

Eneo la washington DC likiwa limejaa barafu                                                                                  

  Zaidi ya watu milioni 50 wameonywa kuwa watarajie barafu ya kina cha zaidi ya futi mbili, itakayoongezeka kutokana na kimbunga na upepo mkali utakaovuma saa chache zijazo.

Comments

Popular posts from this blog

TAZAMA PICHA 30 ZA MREMBO AGNES MASOGANGE AKIJIACHIA KISTAA NJE YA NCHI

Gamboshi: Makao Makuu ya Uchawi na Wachawi yaliyopo Shinyanga, Tanzania

14 parties want Parliament to discuss Zanzibar impasse