Burundi yafanyiwa kikao Addis

 
Burundi yafanyiwa kikao Addis Ababa 


Mabalozi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanafanya mazungumzo kuhusu msukosuko wa Burundi na viongozi wa Umoja wa Afrika katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.

Mkutano huo unafanywa siku moja baada ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa kukutana na rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, ambaye uamuzi wake wa kugombea muhula wa tatu wa uongozi ulizusha miezi kadha ya ghasia.

Mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Samantha Power, alisema mazungumzo hayo hayakufanikiwa kama alivyotaraji.

Rais Nkurunziza alikataa wito wa mazungumzo, upatanishi na kikosi cha Umoja wa Afrika kuingilia kati.

Comments

Popular posts from this blog

TAZAMA PICHA 30 ZA MREMBO AGNES MASOGANGE AKIJIACHIA KISTAA NJE YA NCHI

Gamboshi: Makao Makuu ya Uchawi na Wachawi yaliyopo Shinyanga, Tanzania

14 parties want Parliament to discuss Zanzibar impasse